Klabu za Real Madrid, Chelsea na Manchester United zote zimetajwa kuwania kumsajili mshambuliaji wa Inter Milan, Lautaro Martinez, ambaye anatarajiwa kuondoka Italia baada ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya juzi Jumamosi (Juni 10).

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 amekuwa na msimu bora wa maisha yake ya Inter, akipachika mabao 21 na kutoa pasi saba za mabao kwenye Serie A.

Kwa mujibu wa 90 minutes wawakilishi wa Muargentina huyo wamezungumza na klabu kadhaa kuziarifu kwamba Martinez yuko tayari kwa changamoto mpya msimu huu wa joto.

Chelsea na United, ambazo zimekuwa zikifuatilia maisha ya Martinez kwa miaka mingi sasa, zimeonesha nia ya kutaka kumsajili, lakini italazimika kuzuia nia ya Real Madrid kama ikiwa wanataka kumleta kwenye Ligi Kuu England.

Hata hivyo, Real Madrid imeongeza nia yao katika siku za hivi karibuni huku wakijiandaa kwa marekebisho makubwa katika safu ya ushambuliaji.

Karim Benzema, Eden Hazard, Marco Asensio na Mariano Diaz wote wanaondoka katika klabu hiyo msimu huu wa joto, na kuwaacha Real Madrid wakiwinda wachezaji wengine muhimu.

Mchezaji wa Chelsea Kai Havertz anazingatiwa lakini wasiwasi juu ya bei yake inaweza kuzuia kusajiliwa.

Mshambuliaji anayelengwa na Real Madrid ni Harry Kane wa Tottenham Hotspur, ambaye pia ni kinara wa orodha ya wachezaji wanaotakiwa na Man United.

Spurs wamedhamiria kutomuuza mchezaji huyo wa kimataifa wa England msimu huu wa joto, na hivyo kulazimisha klabu zote mbili kutafuta mahali pengine.

Kwa hiyo, klabu hizo mbili zinachunguza chaguzi zao zote na Martinez, ambaye Inter wanatarajia kuondoka katika klabu baada ya fainali ya Ligi ya Mabingwa, anaibuka kama shabaha nzuri sio tu kwa United na Real Madrid, lakini pia kwa Chelsea.

Kikosi cha Mauricio Pochettino, ambacho kinafuatilia hali ya Kane katika kutafuta mshambuliaji mpya, kiko kwenye mawasiliano ya mara kwa mara na Inter kuhusu masuala mbalimbali, ambayo ni mustakabali wa Romelu Lukaku na kutaka kumnunua kipa Andre Onana.

Apigwa risasi na mumewe kwa kuchelewesha chakula
Wizara ya Elimu yazifunga shule 900, sababu zatajwa