Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga amekunusha madai kwamba atamuunga mkono Makamu wa Rais wa zamani wa Kenya, Kalonzo Musyoka kuwania urais kwenye Uchaguzi wa mwaka 2027.

Odinga ameyasema hayo kupitia msemaji wake kwamba sifa alizompa Musyoka kisiasa siku hazimaanishi  kuwa atamuunga mkono kwenye uchaguzi wa mwaka 2027, kama ilivyokuwa imeripotiwa na baadhi vya Vyombo vya Habari.

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga.

Amesema, ni mapema  kutangaza mgombea urais miaka minne kabla ya kufanyika kwa uchaguzi ingawa kitendo cha kumpa sifa Kalonzo ilitafusiriwa na wengi kwamba huenda mwanasiasa huyo ambaye amewania urais mara kadhaa, atamuunga mkono Kalonzo kwenye uchaguzi ujao.

Hata hivyo, tayari imebainika kuwa vyama tanzu vya muungano wa upinzani havijafurahishwa na kauli ya Odinga kuonesha wazi huenda akamuunga mkono Kalonzo kwenye uchaguzi ujao, hatua inayotishia kusambaratisha upinzani.

Dereva ana haki kujua mwendokasi aliokamatwa nao - Polisi
Wananchi jielekezeni kwenye fursa - Rais Dkt. Samia