Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu wa nchini (TFF), Jamal Malinzi ametuma salam za pongezi kwa Alberto Simago Junior wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Msumbiji (FMF) na Sidiki Tombi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Cameroon (FECAFOOT) kufuatia kuchaguliwa kuwa marais wa mashiriksho ya mpira miguu.

Katika salam zake kwenda FMF na FECAFOOT, Malinzi amesema kuchaguliwa kwao kuogoza mashirikisho hayo kumetokana na imani ya wanafamilia wa mpira miguu.

Kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya TFF na familia ya mpira wa miguu nchini, anawapa pongezi kwa kucgahuliwa kwao.

TFF inaahidi kushirikiana na uongozi mpya wa FMF na FECFOOT katika maendeleo ya mpira wa miguu Afrika na Dunia kote.

Taifa Stars Yaanza Kujifua Dar es salaam
Tz Bara Kushiriki Challenge CUP Mwezi Novemba