Marekani imesema kuwa imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika jaribio lake la kwanza la mtambo wa kutungua makombora ya nyuklia ya masafa marefu.

Mtambo huo wa ardhini umefungwa katika kambi ya kijeshi iliyopo Califonia kwaajili ya kujihami na vitisho ambavyo vimekuwa vikitolewa na maadui zake ikiwemo Korea Kaskazini.

Aidha, Pentagon imesema kuwa jaribio hilo limefanyika baada ya Korea Kaskazini kufanya majaribio yake ya makombora tisa ya masafa marefu mwaka huu hivyo kutishia usalama wa nchi hiyo.

“Mfumo huu ni mhimu sana kwa ulinzi wa taifa letu na jaribio hili ni uthibitisho mkubwa kwamba tuna uwezo wa hali ya juu wa kujilinda na kutetea usalama wa raia wetu,” amesema Mkurugenzi wa kitengo cha ulinzi wa makombora, Admirali Jim Syring.

 

 

Mwakyembe anena mazito baada ya kifo cha aliyechora nembo ya Taifa
?Live: Yanayojiri Bungeni Dodoma leo Mei 31, 2017