Kuelekea mchezo wa Michuano mipya ya Africa Football League, Kocha Msaidizi wa AS Vita ya DR Congo, Roul Shungu amwambia Kocha Mkuu wa Simba SC, Robert Oliveira Robertinho’ kuwa kama kweli wanahitaji kuwaondoa wapinzani wao Al Ahly ya Misri katika michuano basi wanapaswa kuhakikisha wana uwezo wa kuzuia kufungwa nyumbani na ugenini.

Shungu ametoa kauli hiyo kuelekea katika mchezo wa Mkondo wa Kwanza wa michuano hiyo ambao utakuwa ni wa ufunguzi unaotarajia kupigwa kesho Ijumaa (Oktoba 20) kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar.

Shungu ambaye aliwahi kufanya kazi katika klabu ya Young Africans amesema kuwa, kama Simba SC imedhamiria kweli kufanya vizuri katika michuano hiyo basi Kocha Robertinho anapaswa kuwaanda wachezaji wake katika mipango ya kupata ushindi mkubwa nyumbani pamoja na njia za kuweza kuzuia wakiwa ugenini kwani wapinzani wao kawaida hawatabiriki.

“Hii ni hatua kubwa kwa Simba SC kuwa katika timu za kwanza katika michuano hii mipya na bahati ambayo wamepata ni kufungua michuano wakiwa kwenye ardhi ya nyumbani niwapongeze katika hilo japo kuwa wana kazi kubwa mbele ya Al Ahly, nafahamu Simba SC siyo wageni kwenye michuano mikubwa lakini hawatokuwa na mchezo rahisi.

“Ni mkweli kwa sababu ukiangalia kiubora bado Ahly ni bora na wamekuwa na uzoefu mkubwa kushinda Simba SC, nadhani kocha wao hapaswi kuangalia rekodi zitamwambia kitu gani kuweza kupata matokeo anachotakiwa kufanya ni kuwa na mkakati wa kuweza kupata ushindi nyumbani na kisha ugenini maana wapinzani wao kawaida huwa hawatabiriki,” amesema Shungu.

Kasi upigaji vita Kilimo, matumizi ya Bangi yaongezeka
Aliyewalawiti Wanawake watatu yamemkuta