Kampuni ya Sunderland imesema itazindua kwa pamoja jezi zote za Klabu ya Simba za mashindano ambayo wanashiriki kwa msimu wa 2023/24.

Jezi hizo ni za CAF Super League, Ligi ya Mabingwa Afrika, Ligi Kuu Tanzania Bara, Kombe la Shirikisho ‘ASFC’, Ligi Kuu ya Wanawake na Ligi ya Vijana.

Akizungumza na Azam TV, mzabuni aliyeshinda zabuni ya kutengeneza jezi za Simba SC, Sunday Omar amesema tayari jezi hizo zipo nchini na klabu ndio watasema wanazindua lini.

Amemuomba Waziri wa Biashara na Viwanda, Mkurugenzi wa FCC, Polisi na mamlaka nyingine kusaidia kudhibiti jezi ‘Fake’ ili timu zinufaike na mapato yanayotokana na mauzo ya jezi zao.

Sunderland iliingia mkataba Sh bilioni 4 na Simba SC baada wa miaka miwili wenye thamani ya klabu hiyo kumalizana na Kampuni ya Vunja Bei iliyoingia nao miaka miwili iliyopita ukiwa na thamani ya Sh bilioni 2.

Patrick Vieira arudi kwao Ufaransa
Mayele, Young Africans mambo magumu