Seikali imetenga Bilioni 2.5 kwaajili ya ujenzi wa hospitali Mkoani Morogoro. Hayo yamesemwa leo Bungeni wakati Naibu waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI, Selemani Jafo akijibu swali lililoulizwa na mbunge wa Morogoro mjini, Aziz Abood
“Hospitali ya Mkoa wa Morogoro ina tatizo kubwa la msongamano katika wodi ya kinamama ambao wamekuwa wakilala zaidi ya wawili katika kitanda kimoja,. Je, ni lini Serikali itaongeza wodi ya wazazi kwa hospitali hiyo ya rufaa ya mkoa wa Morogoro?” –Â Abood