Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amesema kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini ndiye anayejaribu kupandikiza mgogoro ndani ya chama hicho kwa maslahi yake binafsi.

Ameyasema hayo mapema hii leo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha 360 kinachorushwa na CloudsTv. kilichopo Jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa hakuna haja ya wanachama kuwa na hofu kuwa chama hicho kinaweza kusambaratika hivyo amewataka kuimarisha mshikamano uliopo ndani ya chama hicho.

“Nachojua mimi hakuna mgogoro ndani ya CUF kama inavyoelezwa na baadhi ya watu, isipokuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini anajaribu kupandikiza mgogoro huo kwa maslahi yake binafsi,”amesema Seif.

Aidha, ameongeza kuwa kuna baadhi ya watu ambao wanatumiwa kutaka kukivuruga chama hicho, hivyo amesema kamwe hawatafanikiwa.

Hata hivyo, amesema yeye kama kiongozi ataendelea kufanya shughuli zake za chama na kuwataka walio chini yake wasivunjike moyo.

Cristiano Ronaldo Aandika Rekodi Tano Binafsi
?Live: Yanayojiri Bungeni Dodoma leo Mei 3, 2017