Boniface  Gideon- Tanga.

Mfuko  wa Utamaduni  na Sanaa  nchini,  umetoa  mafunzo  kwa  wasanii  mbalimbali  wa  ndani na nje ya Mkoa wa Tanga  yanayolenga  kuwajengea  uwezo  wa namna  bora  ya  kuchukua mkopo na kurejesha kwa wakati kufuatia Serikali  kutoa Bilioni 20 kwa  mwaka  wa fedha 2023/2024.

Mtendaji  mkuu wa  mfuko  huo, Nyakaho  Mahemba  amewaambia  wasanii hao  kuwa Serikali  imeweka  bajeti  hiyo kwa  lengo  la  kuwawezesha wasanii  kupata  fursa  ya kuchukua mikopo mikubwa ambayo  itawasaidia  kuinuka  kiuchumi.

‘’Rais  Samia anawapenda  sana wasanii na ndio mana  ametoa fedha hizi, mkopo  huu una riba ya asilimia 9 tu na hakuna mkopo ulio na riba nafuu kushinda huu na  uzuri wake  mnaweza  kukopa  kama kikundi  au  mtu mmoja mmoja,  lakini  pia hauna  masharti  mengi  ikiwamo  dhamana ‘’ alisisitiza  Mahemba.

Kwaupande  wake  Kaimu  Katibu  Tawala  Mkoa  wa Tanga,  Sebastian Masanja  aliwataka  wasanii hao  kutumia  fursa  hiyo  ya  mkopo na kuwakumbusha  nidhamu  ya  matumizi  ya  fedha  hizo.

Alisema, ‘’itumieni  fursa hii kwa kuhakikisha mnachukua  mikopo na muwe wabunifu wa miradi ili muinuke  kiuchumi lakini msisahau  nidhamu  ya matumizi ya  pesa hizi mkumbuke huu ni mkopo sio pesa za msaada  unatakiwa uzirudishe tena  kwa wakati,’’ alisisitiza   Masanja.

Laporta ashangaa kinachoendelea Ulaya
Ushirikiano wa kisekta unakuza uchumi - Dkt. Yonaz