Chapisho la hivi karibuni la jarida la Global Peace Index, limetaja nchi 11 ambazo ni hatari zaidi duniani, huku nchi ya Afghanistan ikishika namba moja.

Zingine ni Yemen, Syria, Urusi, Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Iraq, Somalia, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sudan na Ukraine.

Chapisho hilo pia, limefafanua kwamba viwango hivyo vya hatari vimepimwa kutokana na idadi ya vifo vya ukatili, Athari za ugaidi, Uwezo wa nyuklia, Masharti ya amani, Usalama wa jamii, Migogoro ya ndani na Mahusiano ya kimataifa.

Zifuatazo ni baadhi ya sababu ni kwanini nchi hizo zinaonwa kuwa ni hatari zaidi Duniani tukianza na namba moja ambayo ni Afghanistan lakini tukizingatia kwamba na Barani Afrika zipo nchi nne, huku Sudan Kusini ikiongoza.

1. Afghanistan.

Ni nchi hatari zaidi duniani kutokana na migogoro na ukosefu wa utulivu unaoendelea, kwani zaidi ya miongo miwili ya vita imeathiri nchi hiyo, na kuiacha ikiwa na Fahirisi za chini za Maendeleo ya Binadamu duniani.

Mzozo unaoendelea nchini humo, pia umesababisha viwango vya juu vya ghasia na ukosefu wa usalama, huku raia mara nyingi wakibeba mzigo huo.

Hata hivyo, Serikali ya Afghanistan pia inakabiliwa na rushwa, ambayo imefanya kuwa vigumu kutoa huduma za msingi na kuboresha miundombinu ya nchi.

Zaidi ya miongo miwili ya vita imeiathiri Afghanistan na kuiacha ikiwa na mazonge mengi ya kiusalama. Picha ya SABC.

2. Yemen.

Kwa sasa ni nchi ya pili hatari duniani, ikiwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu 2015, na bado hali inaendelea kuwa mbaya zaidi.

Makumi ya maelfu ya watu wameuawa katika mzozo huo, na mamilioni ya wengine wamelazimika kuyahama makazi yao huku huduma za kimsingi kama vile afya na elimu zikiwa haba na njaa imeenea sana katika maeneo mengi.

Vita vya nchini Yemeni, pia vimeruhusu vikundi vya kigaidi kama vile Al-Qaeda na ISIS kupata mkondo wa utulivu kwa baadhi ya maeneo, na kuifanya kuwa hatari zaidi kwa raia.

Yemen ina vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu 2015, na bado hali inaendelea kuwa mbaya zaidi. Picha ya Digital Emigre.

3. Syria.

Ni Taifa ambalo limekuwa katika vita mbaya vya wenyewe kwa wenyewe tangu mwaka 2011. Idadi ya vifo imepita 250,000, na idadi ya wakimbizi wa ndani ni zaidi ya milioni 7.6.

Miundombinu ya nchi hiyo imeharibiwa, na mifumo yake ya afya na elimu iko katika hali mbaya.

Aidha, mzozo nchini Syria pia umesababisha kuongezeka kwa makundi ya kigaidi kama ISIS, ambayo yamefanya mashambulizi ya kikatili kwa raia.

Hata hivyo, ukaribu wa Syria na Ulaya umesababisha mzozo wa wakimbizi wa idadi isiyo kifani. Sababu zote hizi zimeifanya Syria kuwa nchi ya tatu kwa hatari zaidi duniani mwaka 2023 nchi ngumu zaidi kwa raia wa Marekani kusafiri.

Mzozo nchini Syria pia umesababisha kuongezeka kwa makundi ya kigaidi kama ISIS, ambayo yamefanya mashambulizi ya kikatili kwa raia. Picha ya NIP.

4. Urusi.

Ni nchi ya nne kwa hatari zaidi duniani mwaka wa 2023, kutokana na kiwango kikubwa cha mauaji na kuongezeka kwa ukosefu wa utulivu wa kisiasa.

Kiwango cha mauaji nchini Urusi ni cha juu ikilinganishwa na nchi zingine, ni karibu mauaji ya asilimia 9.5 kwa kila watu 100,000.

Hali hii inatokana na viwango vya juu vya umaskini, ukosefu wa usawa pamoja na ukosefu wa utawala wa sheria na rushwa iliyoenea.

Aidha, Urusi pia inakabiliwa na ongezeko la ukosefu wa utulivu wa kisiasa, huku maandamano na vuguvugu la upinzani vikionekana kuwa vya kawaida.

Hali hii, pia inaweza kusababisha kuongezeka kwa ghasia na machafuko ya kiraia katika siku zijazo.

Kiwango cha mauaji nchini Urusi ni cha juu ikilinganishwa na nchi zingine, ni karibu mauaji ya asilimia 9.5 kwa kila watu 100,000. Picha ya Russia Today.

5. Sudan Kusini.

Yenyewe inapatikana Barani Afrika, ikiwa ni nchi ya tano kwa hatari zaidi duniani mwaka 2023. Nchi hiyo imekumbwa na ghasia na vita vya wenyewe kwa wenyewe, tangu ilipopata uhuru wake kutoka kwa Sudan mwaka 2011.

Inaarifiwa kuwa zaidi ya watu 400,000 wameuawa katika vita hivyo na zaidi ya watu milioni 2 wamelazimika kuyahama makazi yao.

Sudan Kusini pia ni nyumbani kwa makundi mengi yenye silaha, ambayo yanafanya kuongezeka kwa ugumu wa upatikanaji wa amani na hivyo kuwa mahali pagumu kuishi.

Zaidi ya hayo, miundombinu ya nchi hiyo pia ipo katika hali mbaya na huduma za msingi kama vile afya na elimu ni chache.

Zaidi ya watu 400,000 wameuawa katika vita nchini Sudan ya Kusini na zaidi ya watu milioni 2 wamelazimika kuyahama makazi yao. Picha ya UN News.

6. Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo – DRC.

Taifa hili limekumbwa na ghasia na migogoro kwa miaka mingi na hali inazidi kuwa mbaya. Serikali haijatulia, na vikundi mbalimbali vyenye silaha vinafanya kazi kote nchini hasa katika eneo la Mashariki.

Pia kuna kiwango cha juu cha umaskini na ukosefu wa usawa, jambo ambalo hurahisisha magenge ya wahalifu na mashirika ya kigaidi kuajiri wanachama wapya.

DRC ni mahali hatari pa kuishi, na kuna uwezekano wa kusalia kuwa moja ya nchi hatari zaidi ulimwenguni kwa miaka mingi ijayo.

DRC ni mahali hatari pa kuishi, na kuna uwezekano wa kusalia kuwa moja ya nchi hatari zaidi ulimwenguni kwa miaka mingi ijayo. Picha ya REUTERS/Djaffar Sabiti.

7. Iraq.

Yenyewe inashika nafasi ya 157 kwenye Fahirisi ya Amani ya Ulimwenguni, ikiwa ni nchi ya saba hatari zaidi duniani, kutokana na migogoro na ghasia zinazoendelea nchini humo.

Matokeo ya Vita vya Iraq, pamoja na migogoro inayoendelea imesababisha mamilioni ya watu kuyahama makazi yao, maelfu ya raia kuuawa na kusababisha mateso makubwa ya wanadamu.

Aidha, Serikali ya Iraq pia imeorodheshwa kama mojawapo ya Serikali fisadi zaidi duniani, jambo ambalo linachangia pakubwa kukosekana kwa utulivu nchini humo.

Migogoro inayoendelea imesababisha mamilioni ya watu kuyahama makazi yao, maelfu ya raia kuuawa na kusababisha mateso makubwa ya wanadamu. Picha ya Arab News.

8. Somalia.

Nchi hii, inashika nafasi ya 156 kwenye Fahirisi ya hivi punde ya Amani ya Ulimwengu na kuifanya kuwa nchi ya nane hatari zaidi duniani.

Somalia imekabiliwa na changamoto kubwa katika miaka ya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa utulivu wa kisiasa, ukosefu wa usalama na umaskini.

Hali ya kibinadamu nchini Somalia ni mbaya, huku zaidi ya watu milioni 6 wakihitaji msaada. Nchi hiyo ina idadi kubwa ya makundi ya kigaidi kama vile Al-Shabaab, ambayo yamefanya mashambulizi dhidi ya raia.

Serikali ya Somalia pia imekuwa ikifanya kazi ya kuboresha hali ya usalama nchini humo na imepata maendeleo katika miaka ya hivi karibuni.

Hata hivyo, kazi kubwa bado inahitajika kuifanya Somalia kuwa salama kwa raia na wageni wanaotembelea eneo hilo.

Hali ya kibinadamu nchini Somalia ni mbaya, huku zaidi ya watu milioni 6 wakihitaji msaada. Nchi hiyo ina idadi kubwa ya makundi ya kigaidi. Picha ya NBC News.

9. Jamhuri ya Afrika ya Kati – CAR.

Kutokana na mzozo unaoendelea na mgogoro wa kibinadamu, Jamhuri ya Afrika ya Kati ni mojawapo ya nchi hatari zaidi duniani, ikiwa inakumbwa na ghasia na ukosefu wa utulivu kwa miaka mingi na hakuna mwisho unaoonekana.

Zaidi ya nusu ya watu wanahitaji msaada wa kibinadamu na mamilioni wamelazimika kuyahama makazi yao kutokana na mzozo huo. Vurugu hizo pia zimesababisha mateso makubwa kwa raia, huku maelfu wakiuawa au kujeruhiwa na wengine kubakwa au kufanyiwa vurugu za aina nyinginezo.

Kutokuwepo kwa usalama CAR, kunamaanisha kwamba watu hawawezi kuendelea na maisha yao ya kila siku bila kuhofia usalama wao na wale ambao wametafuta hifadhi katika nchi nyingine wanakabiliwa na mustakabali usio na uhakika.

Kutokuwepo kwa usalama CAR, kunamaanisha kwamba watu hawawezi kuendelea na maisha yao ya kila siku bila kuhofia usalama wao. Picha ya Atalaya.

10. Sudan.

Ni mojawapo ya nchi hatari zaidi duniani kwa sababu kadhaa ikiwemo kukumbwa na ghasia na migogoro kwa miaka mingi na hali inazidi kuwa mbaya.

Vita vya wenyewe kwa wenyewe vimekuwa vikiendelea nchini humo tangu mwaka 1983, na vimegharimu maisha ya zaidi ya watu milioni 2.

Serikali ya Sudan pia inatuhumiwa kufanya mauaji ya halaiki katika eneo la Darfur, ambayo yamesababisha mamilioni ya watu kuyahama makazi yao.

Aidha, Sudan pia inakabiliwa na makundi yenye itikadi kali kama vile Al-Qaeda na ISIS, ambayo yamekuwa yakihusika na mashambulizi mengi ya kigaidi nchini humo.

Vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan vimekuwa vikiendelea nchini humo tangu mwaka 1983, na vimegharimu maisha ya zaidi ya watu milioni 2. Picha ya Foreign Policy.

11. Ukraine.

Tangu kuanza kwa mwaka 2023, Ukraine inachukuliwa kuwa moja ya nchi hatari zaidi ulimwenguni, kwa sababu ya uvamizi wa Urusi uliofanywa Februari 2022.

Uwepo wa majeshi ya Urusi nchini Ukraine, umesababisha kuenea kwa ghasia na ukiukaji wa haki za binadamu na kuchangia katika cheo cha nchi hiyo katika nafasi ya 153 (kati ya nchi 163 zilizochambuliwa) kwenye Fahirisi ya Amani ya Ulimwenguni.

Tangu kuanza kwa mwaka 2023, Ukraine inachukuliwa kuwa moja ya nchi hatari zaidi ulimwenguni, kwa sababu ya uvamizi wa Urusi uliofanywa Februari 2022. Picha ya NATO.

Hili ni anguko kubwa, kwani Ukraine iliorodheshwa kama nchi ya 33 yenye amani kabla ya uvamizi wa Urusi, wakati huo kulikuwa na kiwango cha chini cha uhalifu na wananchi kwa ujumla walihisi kuwa salama.

Hata hivyo, kutokana na uvamizi wa Urusi na kukaliwa kwa mabavu miji ya Crimea na mashariki mwa Ukraine, hali ya usalama nchini Ukraine imezorota sana.

Jeshi la Urusi, limehusika katika ukiukaji mwingi wa haki za binadamu nchini Ukraine, ikiwa ni pamoja na mateso, ubakaji na mauaji.

Ihefu FC: Hatutasajili kwa mihemko
Man Utd yaanza mawindo kwa Moises Caicedo