Kwa siku kadhaa sasa CUF imekumbwa na mgogoro wa kiuongozi kati ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wake aliyepata kujiuzulu na kurejea tena Profesa Ibrahim Lipumba.
Kwa upande wake, Baraza la Udhamini la CUF kupitia kwa Mwenyekiti wa kikao kilichoketi wiki hii na Mjumbe wa baraza hilo, Peter Malebo alisema mgogoro uliopo ndani ya chama hicho utamalizwa ndani ya chama hicho baada ya kuzikutanisha pande hizo mbili.
“Tatizo lililopo ndani la CUF ni tatizo la muda mrefu na wajumbe wa bodi ya chama hicho ndio wenye jukumu la kumaliza mgogoro huo, lakini mbaya zaidi baadi ya wajumbe wamekuwa ndio wanachonganisha na kukuza mgogoro huo badala ya kuumaliza,” alisema Malebo.
Aidha, Malebo alisema wanampongeza Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kwa kutolea ufafanuzi wa sakata la uongozi wa chama hicho na kumthibitisha Profesa Lipumba kuwa ni Mwenyekiti halali wa chama hicho kwa mujibu wa chama chao.