Kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi kimeendelea kula msoto wa matokeo mabovu, licha ya kumtimua Danny Blind kwenye benchi la ufundi mwishoni mwa juma lililopita.

Uholanzi imeendelea kupoteza katika michezo yake ya kimataifa, baada ya kukubali kufungwa na Italia usiku wa kuamkia leo chini ya kocha wa muda, Fred Grim.

Mchezo huo wa kirafiki ambao ulitarajiwa kuwa na matokeo tofauti kwa Uholanzi, ulimalizika kwa Italia kupata ushindi wa mabao mawili kwa moja.

Hata hivyo, Uholanzi walikua wa kwanza kupata bao kupitia kwa Alessio Romagnoli wa Italia aliyejifunga mwenyewe, kabla ya Eder na Leonardo Bonucci hawajaifungia The Azzuri mabao mawili ya ushindi.

Mchezo huo ulikua unafuatiliwa na aliyekua kocha wa Uholanzi wakati wa fainali za kombe la dunia 2014 Louis Van Gaal ambaye alikua sambamba na kocha Fabio Capello wa Italia.

Mpaka sasa shirikisho la soka nchini Uholanzi halijatoa tamko lolote la kuwa katika mazungumzo ya kuziba nafasi ya Blind, ambayo inatakiwa kumpata mrithi ili kunusuru matokeo yanayokiandama kikosi cha The Orange.

Matokeo ya michezo mingine ya kimataifa ya kirafiki iliyochezwa usiku wa kuamkia hii leo.

Myanmar 0 – 1 India

Georgia 5 – 0 Latvia

Lebanon 2 – 0 Hong Kong

Albania 1 – 2 Bosnia-Herzegovina

Egypt 3 – 0 Togo

Estonia 3 – 0 Croatia

FYR Macedonia 3 – 0 Belarus

Urusi 3 – 3 Belgium

Afrika Kusini 0 – 0 Angola

Morocco 1 – 0 Tunisia

Cameroon 1 – 2 Guinea

Luxembourg 0 – 2 Cape Verde

Austria 1 – 1 Finland

Ireland 0 – 1 Iceland

Ureno 2 – 3 Sweden

Ufaransa 0 – 2 Hispania

Video: Ndege yawaka moto, 141 wanusurika
Mzimu Wa Lionel Messi Waizima Argentina