Mabingwa wa Soka nchini Ufaransa Paris Saint-Germain wanaanda zaidi ya Pauni 80 milioni kwa ajili ya kutuma ofa kwenda Manchester United ili kuipata saini ya Mshambuliaji wa timu hiyo na England, Marcus Rashford katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi.

Inaelezwa kuwa, mabosi wa PSG wanataka kumchukua fundi huyu ikiwa ni sehemu ya kuziba pengo la Mshambuliaji wao Kylian Mbappe ambaye ataondoka mwisho wa msimu huu.

Mbali ya ofa hiyo, pia PSG imepanga kumpa mshahara wa zaidi ya Pauni 500,000 kwa juma, ili kumshawishi zaidi akubali kujiunga nao.

Mkataba wa sasa wa staa huyu unatarajiwa kumalizika mwaka 2028. PSG imekuwa ikiwania saini ya fundi huyu kwa muda mrefu.

Fundi huyu ameonyesha kiwango bora kwenye kikosi cha kwanza cha Man United akiwa mmoja kati ya mastaa tegemeo wa kikosi cha kwanza cha mashetani hao na msimu huu amefunga mabao saba kwenye mechi 34 za michuano yote.

Benchikha: Al Ahly wana presha kuliko sisi
Gamondi: Sina uhakika wa kutwaa ubingwa