Diamond Platinumz anaendelea kupaa katika ulimwengu wa muziki kimataifa ambapo mwaka huu pia nyota yake imeng’aa kwenye tuzo kubwa za Black Entertainment Television (BET 2016).

Mwimbaji huyo ametajwa kuwania kipengele cha Best International Act: Africa akichuana na wasanii wengine nguli Afrika ambao ni pamoja na AKA kutoka Afrika Kusini, Cassper Nyovest wa Afrika Kusini Black Cofee wa Afrika Kusini, Yemi Alade wa Nigeria, Wizkid wa Nigeria, Mzvee wa Ghana na Serge Beynaud wa Ivory Coast.

Diamond BET

Tuzo hizo zitafanyika Juni mwaka huu nchini Marekani ambapo Diamond pia ametajwa kati ya watakaotumbuiza.

Van Gaal Aombwa Kuwa Bosi Wa Jose Mourinho
Simba Wapewa Mbinu Za Kukiboresha Kikosi Chao