Baada ya kusambaa kwa taarifa kwenye mitandao zikieleza kuwa kampuni ya Home Shopping Centre imefunga maduka yake kutokana na kukwepa kodi na kuhusika kwenye sakata la makontena yaliyopotea bandarini, uongozi wa kampuni hiyo umejitokeza na kupinga taarifa hizo.

Kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari, kampuni hiyo imeeleza kuwa habari hizo sio za kweli na kueleza kuwa haijawahi kukwepa kodi na haihusiki kwa namna yoyote na makontena yaliyopotea bandarini.

“Home Shopping Centre Co. Limited haihusiki kabisa kwa njia yoyote ile na wizi, ukwepaji kodi, au potevu wa makontena 349 na yale zaidi ya 2431 yaliyoibuliwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na kamwe haijawahi kujihusisha na uhalifu huo wa kuiba makontena na kukwepa kodi,” ilieleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mfilisi wa kampuni hiyo, Yusufu Mohamed.

Mohamed alieleza kuwa kampuni hiyo ilifunga maduka yake kama ambavyo makampuni mengine hufanya na sio vinginevyo.

Mwanariadha maarufu amuoa mwanamke mwenzake
Mtatiro: Rais Magufuli amenishtua