Mtangazaji maarufu wa burudani nchini Maimartha Jesse,amesema kuwa kuna haja ya Mange Kimabi kurejea nyumbani Tanzania kwakuwa amezaliwa na kukulia hapa .

Akizungumza kwenye EXclusive interview ya Dar 24 ,Maimartha amesema kuwa Hakuna sababu ya Mange kuendelea kuishi ugenini na anatakiwa kurudi nyumbani kwakuwa Tanzania ni nchi huru na kuna mahakama zinatoa haki kwa mtu yeyote .

“Tunaamini yeye ni Mtanzania , na hapa ni kwao inawezekana kama anavyoamini yeye kuna mahali alijichanganya lakini hii ndiyo nchi yake anatakiwa arudi , na Raisi wetu ni mzalendo kama ni mashitaka yatafanyika hii ni nchi huru,” Amesema Mai

Maimartha amefanya uzinduzi wa kipindi chake kipya cha runinga kinachokwenda kwa jina la ICU .

Bofya hapa …. kutazama video

Habari kubwa kwenye magazeti leo, Septemba 5, 2020
Lissu aahidi bima za afya nchi nzima