Bifu jipya limeibuka katika tasnia ya Bongo Flava kati ya rapa Nay wa Mitego na Ommy Dimpoz baada ya wimbo mpya wa ‘Shika Adabu Yako’ wa Nay kuanza kuyasoma masafa ya redio.
Katika wimbo huo, Nay anawashambulia wasanii wengi na kumtaja Ommy Dimpoz akidai mtaani kuna tetesi kuwa ‘jogoo hawiki’.
“Huyu jamaa anajiita Dimpoz, Pose kwa Pose, wanae wanalalamika hawamjui shemeji, mtaani kuna tetesi mwana hapigi mechi, mara oh jogoo hawiki, huwa hawaoneshi shemeji,” anarap Nay wa Mitego kwenye Shika Adabu Yako.
Ommy amevunja ukimya kwa kupost video fupi ya mrembo na kujibu mashambulizi ya Nay wa Mitego.
”
”