Shirikisho la ngumi Tanzania (BFT) limeanda mashindano ya ngumi yaliyofanyika mwishoni mwa juma lililopita  kati ya timu ya Taifa ya Ngumi dhidi ya timu ya Ngome inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) Mashindano hayo yalikuwa ni jaribio la kwanza kwa timu yetu ya ngumi inayoendelea na mazoezo kwa ajili ya maandalizi ya kushiriki Mashindano ya Jumuiya ya Madola yatakayofanyika Gold Coast, AUSTRALIA Aprili 2018. Na yalikuwa pia na lengo la  uzinduzi rasmi wa mazoezi ya kujiandaa na mashindano hayo.

Mashindano hayo ya siku moja yalifunguliwa na Mkurugenzi wa michezo Tanzania ndugu Yusuph Singo.

Timu hiyo ya Taifa iliyo na mabondia wa kiume na kike imeanza vema jaribio hilo la kwanza  baada ya kushinda michezo tisa dhidi ya mitatu walioshinda Ngome kwa upande wa wanaume baada ya kuwa mazoezini tangu mwanzoni mwa mwezi wa nane 2018.

Kwa upande wa mabondia wa kike wote walioshiriki ni kutoka timu ya Taifa.

Matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:-

WANAUME,

  1. Herman Shekivuli (Taifa) alimshinda Issa Kpaya (Ngome) 49 Kgs.
  2. Geoge Costantino (Taifa) alimshinda John Christian (Ngome) 52 Kgs
  3. Ezra Paul (Taifa) alimshinda Emmanuel Marwa ( Ngome) 56 Kgs
  4. Ismail Galiatana (Taifa) alimshinda Fabian Gaudence (Ngome) 60 Kgs
  5. Mohameda Juma (Taifa) alimshinda Isiaka Lusajo (Taifa) 64 Kgs
  6. Kassim Butike (Taifa) alimshinda Julius Nickson (Ngome) 69 Kgs
  7. Selemani Kidunda (Taifa) alimshinda Daudi Kuzenza (Ngome) 75 Kgs
  8. Yusuph Changarawe (Taifa) alimshinda Twalibu Kinyogori (Ngome) 81 Kgs
  9. Haruna Swanga (Taifa) alimshinda Alex Sitta (Taifa)
  10. Alex Michael Ngome) alimshinda Mwalimu Ngayana (Taifa)
  11. Kelvin Kapinga (Ngome) alimshinda Said Ramadhani ( Taifa)
  12. Batele Abed (Ngome ) alimshinda Mwinyi Ally (Huru)

WANAWAKE

  1. Siwatu Kimbe (Taifa) alimshinda Lusiana Gadani (Taifa)
  2. Safina Fussi (Taifa) alimshinda Asha Juma (Taifa)
  3. Najma Isike (Taifa) alimshinda Monica Malango (Taifa)
  4. Mariam Macho (Taifa) alimshinda Naomi Shoo Taifa)
  5. Grace Mwakamale (Taifa) alimshinda Leonia Kalimunju ( Taifa)

Aidha wakati wa kufungua mashindano hayo Mkurugenzi wa michezo Yusuph Singo alisema serikali imeona na  inatambua  jitihada zinazofanywa na  BFT katika kuendeleza mchezo wa Ngumi Tanzania na hasa hatua za kuandaa timu ya Taifa mapema kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola 2018.

Alisema serikali itakuwa karibu na BFT kuhakikisha mazoezi hayo yanaendelea vizuri na kusaidiana kuondoa changamoto zilizopo.

Alieleza kuwa kwa hivi sasa serikali ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha mpango wa timu ya Taifa ya ngumi kwenda nchini Cuba kwa ajili ya mazoezi ya kushiriki mashindano ya Jumuya ya madola 2018.

BFT pia imeahidi kuwa mashindano hayo yatakuwa yanafanyika kila wa kila  mwezi kwa kushindana na timu za ndani na nje ya Tanzania.

Lema, Nassari wawasilisha ushahidi Takukuru
Haji Manara atupa kombora nyumba ya jirani