Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji ya Ligi Kuu ya Bodi ya Ligi ‘TPLB’ imemfungia Michezo mitatu na kumtoza Faini ya Shilingi 500,000, Beki wa Kushoto wa Simba SC Gadiel Michael kufuatia kosa la kuvunja Kanuni.

Taarifa iliyotolewa na Bodi ya Ligi ‘TPLB’ imeeleza kuwa mchezaji huyo alivunja kanuni za Ligi Kuu kwa kosa la kulazimisha kuingia Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, saa 4:25 asubuhi, siku ya mchezo dhidi ya Mbeya City uliomalizika kwa sare 1-1 kwa kile alichoeleza alitaka kukagua kiwanja.

Hata hivyo imeelezwa kuwa Gadiel Michael ambaye alikuwa ameongozana na watu kadhaa waliovalia fulana zenye nembo ya klabu ya Simba, alikatazwa kuingia Uwanjani hapo kwa muda huo na walinzi, lakini alitumia hila na kufanikiwa kuingia.

Mchezaji huyo alipoingia Uwanjani hakuonesha dalili yoyote ya kukagua eneo la kuchezea na badala yake alionekana kwenda moja kwa moja hadi eneo la katikati ya kiwanja na kumwaga vitu vyenye asili ya unga.

Wakati huo huo Kamati ya usimamizi wa Ligi (TPLB) imeitoza klabu ya Simba faini ya Sh. 1,000,000 (milioni moja) kwa kosa la baadhi ya wachezaji wake kuingia uwanjani kwa kupitia mlango usio rasmi kuelekea mchezo wa sare ya 1-1 dhidi ya Mbeya City uliofanyika kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya Novemba 23, 2022.

Simba walilazimisha baadhi ya wachezaji wao waruhusiwe kuingia uwanjani kupitia mlango wa kuingilia jukwaa la watu maalum na walipozuiwa na walinzi wa uwanjani (stewards), Simba walitumia nguvu kutimiza nia yao.

Nasreddine Nabi kuikosa Tanzania Prisons
Mradi kuboresha matibabu ya dharula wazinduliwa