Ligi Daraja la Kwanza nchini (FDL) raundi ya 13 inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa timu 24 [kucheza michezo 12 katika viwanja tofauti, huku kundi A na C kukiwa na ushindani mkali kwa kila timu kuwania kupanda ligi kuu ya Vodacom msimu ujao.

Kundi A, African Lyon watawakaribisha Polisi Dar katika uwanja wa Mabatini – Mlandizi, Ashanti United dhidi ya KMC uwanja wa Karume, huku Jumapili Kiluvya wakiwakaribisha Polisi Dodoma uwanja wa Mabatini – Mlandizi na Friends Rangers wakicheza na Mji Mkuu uwanja wa Karume jijini Dar es salaam.

Kesho Jumamosi, Kundi B Polisi Morogoro watacheza dhidi ya Njombe Mji uwanja wa Jamhuri, Morogoro, Kurugenzi FC dhidi ya JKT Mlale uwanja wa Wambi – Iringa, Burkinafaso dhidi ya Lipuli na Kimondo watawakaribisha Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Vwawa – Mbozi.

Kundi C, Polisi Mara FC watawakaribisha Panone FC uwanja wa Karume mjini Musoma, Geita Gold watacheza dhidi ya JKT Oljoro uwanja wa Nyankumbu mjini Geita, JKT Kanembwa watakua wenyeji wa JKT Oljoro uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma, huku Rhino Rangers wakicheza dhidi ya Mbao FC uwanja wa Ali Hassani Mwinyi mjini Tabora.

Soka La China Laanza Kutishia Amani Ya Biashara Ya Wachezaji
Mbowe atangaza baraza la Mawaziri Kivuli, msikilize hapa