Arsenal itaimarika kwenye mchezo wao wa Premier League Jumapili hii dhidi ya Chelsea kufuatia kupona kwa wachezaji wake muhimu Mesut Ozil na Alexis Sanchez.
Kama vile hiyo haitoshi, Wenger atafaidika pia na kurejea kwa Tomas Rosicky, Danny Welbeck, Francis Coquelin na Jack Wilshere ambao wanatarajiwa kurejea dimbani mwezi ujao.
Hata hivyo Chelsea nao wanatarajiwa kuimarika kwa kurejea kwa Eden Hazard katika mchezo huo utakaochezwa Emirates.
Mesut Ozil yuko fiti kurejea uwanjani.
Alexis Sanchez naye amepona na yuko tayari kuikabili Chelsea