Umoja wa Afrika umesema kwamba mataifa ya Afrika yaimarishe mahakama zake na kupanua uwezo wa mahakama ya Afrika kuhusu haki na haki za binaadamu.

Hayo ni kufuatia umoja huo kuunga mkono mpango wa kujiondoa kwa pamoja katika mahakama ya ICC ambayo mataifa mengi ya Afrika yanahisi inawalenga viongozi wa bara la Afrika pekee.

Viongozi wa Afrika wamesema kuwa mahakama hiyo ilikosea kumlenga rais wa Sudan Omar El Bashir kwa mauaji ya Darfur na Uhuru Kenyatta wa Kenya kwa kuchochea ghasia za baada ya uchaguzi.

Mpango huo unapendekeza kwamba mataifa ya Afrika yanafaa kuimarisha mahakama zake na kupanua uwezo wa mahakama ya Afrika kuhusu haki na haki za binaadamu.

McGregory amtosa rasmi Mayweather, Kuzichapa na Pacquiao
Serikali yaendelea na msimamo wake kuhusu pori la Selous