Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amempokea Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili Zanzibar katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Mhe. Scotland yupo nchini kwa ziara maalumu ya kukutana na kumfahamisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan maudhui ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Madola unaotarajiwa kufanyika nchini Rwanda mwezi Juni 2022.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimpokea Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimkaribisha Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar  
Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar 
Mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland yakiendelea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar 

SIMULIZI: Mwanangu alikuwa haelewi kitu darasani
Young Africans yaanza safari ya Dar es salaam