Ligi kuu ya soka nchini England iliendelea tena usiku wa kuamkia hii leo kwa michezo kadhaa kuchezwa, ambapo vinara Chelsea walikua nyumbani kwa Sunderland (Stadium Of Lights) wakisaka point tatu muhimu.
Bao la kiungo kutoka nchini Hispania Cesc Fabregas, lilitosha kuwapa ushindi The Blues na kujikita kileleni kwa tofauti ya point sita dhidi ya wapinzani wao.
Ushindi huo kwa Chelsea unakuwa wa kumi mfululizo, hali ambayo inaendelea kudhihirisha ubora wa kikosi kinachonolewa na meneja kutoka nchini Italia Antonio Conte.
Matokeo ya michezo mingine ya ligi ya nchini England iliyochezwa usiku wa kuamkia hii leo.
Middlesbrough 0 – 3 Liverpool
West Ham United 1 – 0 Burnley
Crystal Palace 1 – 2 Manchester United
Manchester City 2 – 0 Watford
Stoke City 0 – 0 Southampton
Tottenham Hotspur 3 – 0 Hull City
West Bromwich Albion 3 – 1 Swansea City