Msanii Hussein Machozi ameikataa kauli ya watu wanaomsema amefungiwa ndani na mwanamke nchini Italia huku wengine wakimwambia kwamba yeye ndio ameolewa na mwanamke huyo.

Akizungumzia hilo kupitia EATV & EA Radio Digital Hussein Machozi amesema watanzania wanapenda sana maneno hasa wakiona mtu anaishi nje ya nchi au kupata mwanamke aliyemzidi kipato.

“Watanzania wakiona mtu amepata mwanamke mwenye pesa utaambiwa umeolewa, Ben Pol aliambiwa kaolewa na mwanamke Mkenya na Dogo Janja nae aliambiwa ameolewa na Irene Uwoya, hawajui mtu ametoka nae wapi wanasema ameolewa, mimi nilienda Ulaya kwa mambo yangu,” ameeleza Hussein Machozi

“Hakuna mwanaume anayeolewa wanaume wote wanaoa, Mtanzania huwa hataki kuona mtu anafanikiwa, maneno yao huwa wanayatoa Instagram wanaamini mtu akienda Ulaya anaenda kuishi vizuri,” ameongeza Machozi.

Msanii huyo amekuwa akiishi nchini Italia kwa kipindi cha miaka 7 ambapo amefanikiwa kupata mwanamke na mtoto mmoja wa kike.

Habari kubwa kwenye magazeti leo, Mei 31, 2021
Waziri Mkuu wa Uingereza afunga ndoa