Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amekubali kushindwa katika mbio za kuwania nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa baada ya timu yake kutoka sare ya 1-1 na Aston Villa Jumamosi (Mei 20), akisema hawajaharibika sana na kufurahia Ligi ya Europa msimu ujao.

Baada ya kuangusha alama mbili kwenye uwanja wa Anfield, Liverpool wanahitaji kushinda mchezo wao wa mwisho dhidi ya Southampton, na wanapaswa kuombea Manchester United au Newcastle United kutopata alama hata moja katika mechi mbili walizosalia nazo.

“Tutaifanya Ligi ya Europa kuwa shindano letu,” amesema Klopp akiiambia BBC Sport.

“Sijakosea kiasi hicho. Kwamba tayari tumefuzu kwa Ligi ya Europa ni jambo la kushangaza kwa timu hizi zote zinazotuzunguka. Hiyo ni ngumu sana na tulifanya hivyo, ni nzuri.

“Kwa muda mrefu hatukuweza hata kusikia sauti ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, hivyo ndivyo tulivyokuwa mbali. Ligi ya Ulaya iko sawa kabisa. Hebu tuone tunachoweza kufanya.”

Jacob Ramsey aliifungia Villa bao la kuongoza katika kipindi cha kwanza na wakaweza kuwaweka pembeni wenyeji kwa muda mwingi wa mechi.

Hata hivyo, umati wa watu wa Anfield ulilipuka pale Mbrazil Roberto Firmino alipotoka kwenye benchi na kufunga bao la kusawazisha dakika ya 89 katika mechi yake ya mwisho ya nyumbani akiwa na Liverpool baada ya misimu nane ya kukaa hapo.

Liverpool hawakuweza kupata ushindi wa kuchelewa zaidi, lakini Klopp alisema ameridhishwa na matokeo kutokana na timu yake ilivyokuwa wiki chache zilizopita.

“Ni sare na ni sawa,” amesema Klopp akiwaambia waandishi wa habari.

Maafande wa Polisi wazitisha Simba SC, Azam FC
Mashine ya kisasa ya kukaushia Nafaka yazinduliwa