Boniface Gideon – Tanga.

Wakazi wa Vijiji Vitano kati ya tisa vilivyopo Kata ya Boma Wilayani Mkinga Mkoani Tanga, wamenufaika na Mradi wa utunzaji wa Rasilimali Bahari, unaosimamiwa na Shirika la Mwambao la Coastal Community Network Tanzania – CFMA, baada ya kukabidhiwa Boti kwa ajili ya kuongeza ulinzi shirikishi kwa jumuiya za usimamizi wa Rasilimali Bahari za na BMU.

Afisa Mtendaji Mkuu wa CFMA, Said Khalid amesema Boti hiyo yenye thamani ya Mil.35 imetolewa kwa Vijiji vya Boma kichakamiba, Mwaboza, Boma Subutuni, itasaidia kulinda Rasilimali Bahari na kuzuia uvuvi haramu, na imekabidhiwa ikiwa ni miezi michache baada ya Wavuvi na wakazi wa Vijiji hivyo kupatiwa Elimu ya Ufugaji wa miamba Bahari.

Mkuu wa Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga Kanali Maulid Surumbu ( kulia) akikabidhi hati ya Mkataba wa Boti ya Ulinzi Shirikishi kwa Mwenyekiti wa Jumuiya za Usimamizi wa Rasilimali Bahari BMU Wilayani humo Kassimu Alfan,Boti hiyo imetolewa na Shirika la Mwambao Coastal Community Network Tanzania kwaajili ya kusaidia Ulinzi Shirikishi kwa Vijiji 5 vya kata ya Boma.

Akipokea msaada huo, Mkuu wa Wilaya ya Mkinga, Kanali Maulid Surumbu amelishukuru Shirika Hilo na kuwataka Wadau mbalimbali kuendelea kuisaidia Jamii ya Mwambao wa Bahari, ili Matumizi ya Bahari yaweze kuleta matokeo chanya ya Kiuchumi kwa wakazi.

Amesema, ‘kwa niaba ya Wakazi wa Wilaya ya Mkinga tunatoa Shukrani Sana kwa msaada huu tunawaahidi kuwa msaada huu utatumika kama ilivyokusudiwa , niwaombe Wakazi wa Boma hususani Wavuvi nendeni mkaitumie Boti hii kwa malengo yaliyokusudiwa na si vinginevyo.”

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Mwambao Coastal Community Network Tanzania Said Khalid (mwenye kipaza sauti) akikabidhi Boti ya Ulinzi Shirikishi kwa Jumuiya za Usimamizi wa Rasilimali Bahari kata ya Boma wilayani Mkinga mkoani Tanga.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya za Usimamizi wa Rasilimali Bahari – CFMA (BMU), Wilaya ya Mkinga, Kassimu Khalfan amesema awali kabla ya kupokea msaada huo walikuwa wanatumia Mitumbwi na Majahazi kufanya doria za Ulinzi Baharini, Hali iliyowawia vigumu kuwapata wahalifu,

“Awali tulikuwa tunateseka Sana kufanya Ulinzi Baharini kutokana na kukosa Vifaa vya kisasa kwakuwa wahalifu Wengi wa Baharini wanatumia Boti za kisasa hivyo ilikuwa ni vigumu kuwakamata kirahisi lakini kwasasa tutawakamata kwa urahisi kwakuwa tunavifaa vya kisasa zaidi,” alisema Khalfan.

KMC FC yaomba radhi kwa kichapo
Robertinho awatuliza mashabiki Simba SC