Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekutana na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ili kuimarisha uhusiano na kubadikishana uzoefu katika kuboresha utekelezaji majukumu ya tume hizo.

Baadhi ya mambo ya ambayo tume hizo zinashirikiana ni utekelezaji wa mkakati wa utoaji wa elimu ya mpiga kura na marekebisho ya Sheria mbalimbali.

Mkutano huo wa siku mbili unafanyika mjini Unguja na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka  pande zote mbili na kuongozwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Bw. Kailima Ramadhani.

Katika mkutano huo Bw. Kailima ilieeleza jinsi NEC ilivyoshiriki katika kutoa elimu ya mpiga kura na kuelimisha wadau wa uchaguzi na wananchi juu ya taratibu za uchaguzi na majukumu ya Tume hiyo kikatiba.

Alisema NEC inatekeleza mkakati wa kutoa elimu ya mpiga kura kwa kushiriki kwenye maenesho na mikutano mbalimbali na imefanikiwa kukutana ana kwa ana na wadau na wananchi.

Aliongeza kuwa kupitia mkakati huo NEC ilishiriki maonesho ya Sabasaba na Nanenane, mkutano mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) na kutembelea shule za Sekondari kwa lengo la kutoa elimu ya mpiga kura.

Kwa upande wake  Mkurugenzi wa Uchaguzi wa ZEC Bw. Salum Kassim Ali. alisema Tume hiyo inaendelea na marekebisho ya Sheria ya Tume ambayo kupitia mchakato wa marekebisho hayo imepata uzoefu ambao unaweza kuisaidia tume hizo katika kuboresha utekelezaji wa majukumu yake.

Alisema pamoja na kufikia hatua hiyo, ZEC iko kwenye hatua ya mwanzo ya kutoa elimu ya mpiga kura hivyo uzoefu ulioupata NEC itaisaidia ofisi yake kuboresha utoaji wa elimu ya mpiga kura kwa upande wa Zanzibar.

Bw. Ali alifafanua kuwa kwa upande mwingine anaamini NEC itajifunza mengi kutokananna hatua iliyofikiwa na ZEC katika kufanya marekebisho ya Sheria ya Tume ya Uchaguzi.

Mkutano huo kati ya NEC na ZEC unatarajia kutoka na mapendekezo ambayo yanaziunganisha tume hizo katika kufikia malengo yaliyowekwa kikakitaba.

Ni Dhidi Ya Stand United Ijumaa Hii
Joey Barton Haishiwi Vituko