Kikosi cha Simba SC kimewasili salama mjini Lilongwe-Malawi tayari kwa mchezo wa Mkondo wa kwanza wa Hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika dhidi ya Nyassa Big Bullets.

Simba SC ilianza safari jijini Dar es salaam-Tanzania mapama leo Alhamis (Septamba 08) Alfajiri ikiwa na Kocha Mkuu wa Muda Juma Mgunda ambaye atasidiana na Kocha Seleman Matola, baada ya kuondoka kwa Kocha Zoran Maki.

Kwa mujibu wa kurasa za Mitandaio ya Kijamii za Simba SC, Kikosi cha Simba SC kimewasili mjini Lilongwe asubuhi hii, na kitacheza mchezo wake dhidi ya Nyasa Big Bullets Jumamosi (Septamba 10).

Muswada taarifa binafsi kuwafikia Wabunge
Matatani kwa 'kuishika sharubu' Serikali