Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Ellen Mkondya kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Hospitali ya Taifa – Muhimbili, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Benjamini Mkapa.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus imeeleza kuwa, pia Rais Samia amemteua Justine Peter Mwandu, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Bima la Taifa (NIC). ambaye ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Tanzania Reinsurance (TANRE).

Aidha, pia Rais memteua Prof. Verdiana Grace Masanja kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI). Masanja ni Profesa wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela na teuzi zingine ni kama inavyoonekana katika taarifa hapo chini.

Richard jela miaka 30 kwa ubakaji
Saba kizimbani kwa mauaji ya Askari, kujeruhi