Timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ imewashangaza vijana wa timu ya Taifa ya Ghana (U17) baada ya kuchomoa mabao mawili katika dakika za nyongeza na kupata sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Mchezo huo ni wa mwisho kwa Serengeti hapa nchini kwani Aprili 5 timu hiyo itaondoka kuelekea Morocco kwa ajili ya kambi ya mwezi mmoja kabla ya kwenda Gabon kwenye michuano ya Afrika kwa vijana itakayoanza mwezi ujao.

Sulley Ibrahim aliipatia Ghana bao la kuongoza dakika ya 21 kwa shuti kali ndani ya 18 lililomshinda mlinda mlango wa Serengeti Ramadhan Kabwili na kutinga wavuni.

Katika mchezo huo wachezaji wa Serengeti walikuwa wakicheza taratibu huku mipango yao ikishindwa kutimia mara kwa mara baada ya kuzidiwa ujanja na vijana wa Ghana.

Arko Mensah aliipatia bao la pili Ghana kwa mpira wa adhabu ndogo nje kidogo ya 18 alioupiga kiufundi na kutinga moja kwa moja wavuni.

Serengeti walisawazisha mabao hayo katika dakika za nyongeza kupitia kwa Assad Juma kwa mkwaju wa penalti kabla Muhsin Malima hajafunga bao la pili mwishoni kabisa mwa mchezo.

Magazeti ya Tanzania leo Aprili 4, 2017
Crystal Palace Kuzungumza Na Zaha