Kocha wa Timu ya Taifa ya Cameroon Rigobert Song amekanusha taarifa za kumtimua Mlinda Lango Andre Onana, kwa sababu za kukataa kutii amri ya kutimiza jukumu la ushirikiana na kupinga mpango wa Rais wa Shirikisho la Soka nchini humo Samuel Eto’o kufanya mazoezi ya timu hiyo.

Onana aliondolewa kwenye kikosi cha Cameroon saa chache kabla ya mchezo pili wa Kundi G dhidi ya Serbia uliomalizika kwa timu hizo kufungana 3-3.

Song amesema amelazimika kumuondoa Mlinda Lango huyo wa klabu ya Inter Milan ya Italia, kwa sababu za kinidhamu ambazo zilipelekea washindwe kuelewana, hasa alipokataa kucheza mchezo dhidi ya Serbia jana Jumatatu (Novemba 28).

“Ni mchezaji muhimu, lakini tuko kwenye michuano migumu, hivyo ni bora akatupisha ili tumalize hili kwanza,”

“Ninajua ninachopaswa kufanya, na hiyo ni kuhakikisha kuwa timu kwanza halafu mchezaji baadae.” alisema kocha huyo baada ya mchezo dhidi ya Serbia

Alipoulizwa na Shirika la Habari la AFP iwapo angeanza mchezo wa jana dhidi ya Serbia badala ya Onana, Mlinda Lango namba mbili Devis Epassy alijibu “Ningependa hili swali aulizwe Kocha Song, mimi sitakua tayari kujibu”

Ninachojua hakuna tatizo lolote katika kambi yetu hapa QATAR.” alisema Devis Epassy

FA CUP: Chelsea yarudishwa Ettihad Stadium
Juventus FC yatikisika, Bodi yajiuzulu