Rais wa Marekani Donald Trump ametimiza siku mia moja tangu achaguliwe na kuwa Rais wa Marekani ambapo amefanya maadhimisho kwa kuhudhuria dhifa ya chakula cha jioni na wanahabari katika Ikulu ya White House.

Katika maadhimisho hayo Rais Trump ametoa hotuba ya kushambulia wanahabari ambapo amelinganisha na kutofautisha siku mia moja za uongozi wake kuwa ni siku mia moja za wanahabari kushindwa na kazi yao’, na kutetea mafanikio yake.

Akihutubia umati mkubwa katika jimbo la Pennsylvania, Rais Trump amesema amekuwa akitimiza ahadi zake kila siku, hususan kurejesha kazi za viwanda na kumaliza mzozo katika sekta ya makaa ya mawe.

Aidha, Rais Trump amewaaambia wafuasi wake huko Pennsylvania kwamba ameridhika kuwa pamoja nao katika dhifa hiyo.

Mrema awaasa wananchi kumrudia Mwenyezi Mungu
Video: JPM, Majaliwa msafara mzito anga za Mbowe, Janga jipya kwa wenye vyeti feki