Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kinachodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, kitafanya mazoezi leo jioni saa 1 Algeria, sawa na saa 3 usiku kwa saa za Afrika Mashariki katika uwanja wa Mustapher Tchaker utakaotumika kwa mchezo wa kesho dhidi ya wenyeji Algeria.

Stars inayonolewa na kocha mzalendo, Charles Boniface Mkwasa iliwasili salama jana jioni katika mji wa Blida, uliopo takribani kilometa 75 kutoka katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Houari Boumediene jijini Algiers.

Mkwasa amesema mchezo wa kesho watajituma kadri ya uwezo kuhakikisha wanapata ushindi, makosa yaliyojitokeza katika mchezo wa awali yamefanyiwa kazi na anaamini vijana wake watapambana kusaka ushindi katika mchezo huo.

Wachezaji wote 21 wapo katika hali nzuri, hakuna mchezaj majeruhi hata mmoja, hivyo kocha Mkwasa ana wigo mpana wa kumtumia mchezaji yoyote anayemuhitaji kwa ajili ya mchezo huo wa kesho.

Mchezo huo wa kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia nchini Urusi mwaka 2018, utachezeshwa na waamuzi kutoka nchini Mali na utaanza saa 1:15 usiku (Algeria) sawa na saa 3:15 usiku kwa saa nyumbani Tanzania na Afrika Mashariki.

Mchawi Messi Akiri Kuitamani Arsenal Ya Wenger
Kibadeni Aanika Kikosi Cha Kilimanjaro Stars