Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. James Mdoe amesema Serikali Nchini inatambua mchango unaotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China katika miundombinu ya barabara, kukuza biashara na elimu na kujenga uwezo wa sekta ya kilimo barani Afrika.

Prof.Mdoe ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 13 wa China-Africa uliofanyika jijini Dar es salaam na kuhusisha watafiti na Wataalamu wabobezi kutoka vyuo vikuu katika mataifa mbalimbali barani Afrika wakati ambapo Tanzania na China zinaadhimisha miaka 60 ya uhusiano wa kidiplomasia.

Amesema, Serikali ya China kwa muda mrefu imekuwa ikitoa mchango mkubwa kwa kujali elimu katika sayansi na teknolojia kwa kujenga uwezo wa sekta hiyo katika bara zima la Afrika, na kwqmba Novemba, 2021 kwenye sherehe za ufunguzi wa Mkutano wa nane wa Mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika, Rais Xi Jinping wa China alitangaza kushirikiana na nchi za Afrika kutekeleza programu tisa, ikiwa ni pamoja na ile ya kujengea uwezo bara la Afrika.

Xi alisema China itasaidia kujenga au kuboresha shule 10 barani Afrika, na kuwaalika wataalamu 10,000 wa ngazi ya juu wa Afrika kwenye semina na warsha ikiwa ni pamoja na kuahidi kutatekeleza Mustakabali wa Afrika- mradi wa ushirikiano kati ya China na Afrika kwa elimu ya ufundi stadi”, na kuanzisha mpango wa ajira “kupitia treni” kwa wanafunzi wa Kiafrika nchini China.

Prof. Mdoe amesema China itaendelea kushirikiana na nchi za Afrika kuanzisha “Warsha za Luban”, na kuhimiza makampuni ya China barani Afrika kuunda angalau nafasi za kazi 800,000 kwa wazawa kupitia makampuni yao yanayopata nafasi za uwekezaji na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo barani Afrika.

“Hadi sasa, China imetoa zaidi ya ufadhili wa masomo 2000 na maelfu ya fursa za mafunzo ya ufundi stadi kwa Tanzania, na kuendelea kuwafundisha wenyeji lugha na utamaduni wa Kichina, ujuzi wa vitendo na ujuzi wa kitaalamu kupitia majukwaa kama vile Taasisi ya Confucius, na usaidizi wa kiufundi,” alisema.

China pia imesaidia kujenga Shule mbili za Msingi za Urafiki kati ya China na Afrika kwa Tanzania, Kituo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi mkoani Kagera na maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambayo ni miongoni mwa maktaba kubwa na yenye vifaa bora zaidi barani Afrika alisema.

Aidha akikumbushia hotuba ya Rais Xi katika Mkutano wa 15 wa BRICS, ambao ulifanyika Agosti 2023 huko Johannesburg, Afrika Kusini kwa Viongozi wa China na Afrika alitumia fursa hiyo kutangaza mipango mitatu yenye umuhimu mkubwa kwa maendeleo ya Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Maendeleo hayo ni pamoja na Kusaidia Ukuzaji wa Viwanda barani Afrika, Kusaidia Uboreshaji wa Kilimo wa Afrika na Ushirikiano wa China na Afrika katika Ukuzaji wa Vipaji kwa ustawi wa nchi nyingi za kiuchumi barani Afrika na ushirikiano wa vitendo kati ya Afrika na China.

Naye Balozi wa China nchini Tanzania, Chen Mingjian amesema mkutano huo ni muendelezo wa sherehe za Tanzania na China zinaadhimisha miaka 60 ya uhusiano wa kidiplomasia na kuhusisha na sherehe za kongamano la 13″ China-Africa wataalamu Wabobezi na watafiti kutoka bara la Afrika Na China.

Amesema pia wataangalia jinsi ya kuongeza soko la watalii kwani katika kipindi hiki cha hivi karibuni watalii kutoka China wameongezeka nchini tofauti na miaka ya zamani.

Wazalendo huru wawagusa Wanawake wafungwa
GGML yatoboa siri kuongeza idadi ya Wanawake kwenye madini