1. Umati wa Waandamanaji wapatao 5,000 hadi 10,000 walikusanyika katika kituo cha polisi siku hiyo.

2. Lengo la maandamano hayo lilikuwa ni kuishinikiza Serikali ya ubaguzi wa rangi kusitisha sheria zinazowataka Waafrika kubeba pasi kila wakati.

3. Vyanzo havikubaliana kuhusu nia ya umati, baadhi wanaeleza kuwa umati wa watu ulikuwa wa amani huku wengine wakieleza kuwa umati huo ulikuwa ukiwarushia mawe Polisi na kwamba risasi zilianza wakati umati huo ulipoanza kuelekea kwenye uzio unaozunguka kituo cha Polisi.

4. Kulikuwa na majeruhi 289 kwa jumla, wakiwemo watoto 29.

5. Watu wengi walipata majeraha ya mgongo kwa kupigwa risasi walipokuwa wakikimbia.

6. Ripoti ya Polisi ya mwaka 1960 ilidai kwamba maafisa wa Polisi wachanga na wasio na uzoefu waliogopa na kufyatua risasi moja kwa moja, na kusababisha athari ya mnyororo ambayo ilidumu kama sekunde arobaini.

7. PAC na ANC zilikuwa zikigombea kuungwa mkono na watu, na PAC ilipata upepo wa maandamano ya kupinga pasi ya ANC, yaliyopangwa kufanyika tarehe 31 Machi. kwanza waliamua kugoma na kupanga maandamano yao kwa siku 10 mapema.

8. Tume ya Ukweli na Maridhiano, iliyoundwa mwaka 1995 kuchunguza ukatili uliofanywa kwa pande zote mbili wakati wa miaka ya ubaguzi wa rangi, iligundua kuwa vitendo vya Polisi ndivyo vilivyosababisha mauaji hayo.

9. Wakati Afrika Kusini ilipofanya uchaguzi wake wa kwanza wa kidemokrasia, huku Nelson Mandela akichaguliwa kuwa Rais wake wa kwanza wa kidemokrasia, Machi 21, Siku ya Haki za Kibinadamu ilitangazwa rasmi kuwa sikukuu ya umma.

10. Rais wa zamani Nelson Mandela alitia saini Katiba mpya Desemba 1996 huko Sharpeville.

TMX wapaisha mapato Kagera
MAKALA: Kesho kuna matumaini zaidi kuliko jana