Mgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye anaongoza katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa rais, ambao ulifanyika baada ya miaka kadhaa ya ghasia na mzozo wa kisiasa.

Mshindi wa uchaguzi huo atakuwa na jukumu la kuiongoza Senegal, inayotazamwa kama kinara wa demokrasia katika eneo la Afrika Magharibi, lililokumbwa na matukio ya mapinduzi, kuiondoa katika matatizo yake ya karibuni na kusimamia mapato kutoka kwa hifadhi za mafuta na gesi ambazo zinatarajiwa kuanza uzalishaji hivi karibuni.

A Senegalese supporter holds a poster of jailed Senegalese opposition leader Ousmane Sonko during an electoral campaign caravan to support a detained presidential election candidate Bassirou Diomaye Faye, who Sonko picked to replace him in the race, in the outskirts of Dakar, Senegal March 12, 2024. REUTERS/Zohra Bensemra

Faye alikuwa amewaahidi wapiga kura mabadiliko makubwa na ya kweli na ameonekana kupata uongozi wa mapema dhidi ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa muungano unaotawala Amadou Ba.

Wagombea saba kati ya 17 wa urais wamempongeza Faye mwenye umri wa miaka 44 kutokana na dalili za mwanzo za kura nyingi alizopata zinazoendelea kuhesabiwa na kutangazwa kupitia vituo vya kuhesabia kura na yaliyochapishwa na vyombo vya Habari vya nchini humo.

Willy Onana aahidi mazito safari ya Nusu Fainali
Joao Cancelo: wamenikosea heshima