Johansen Buberwa – Kagera.

Wanafunzi wanaotarajia kuhitimu  masomo ya kidato cha Sita katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera wamehimizwa kutumia vizuri elimu waliyoipata kipindi walipokuwa shuleni, ili kuleta mabadiliko katika jamii inayowazunguka na kujiepusha na makundi yasiyofaa hasa wakati watakaokuwa wakisubiri Matokeo ya mitihani yao.

Rai hiyo imetolewa na Mgeni rasmi ambaye Mwenyekiti wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi – UCCM, Bukoba Mjini, James Nyamanza katika Mahafali ya Kidato cha Sita ya umoja wa Wanafunzi Wasabato Kanda ya Bukoba Mjini – ASSA, ambayo yamefanyika shule ya Sekondari Nyakato.

Amesema, Wanafunzi hao wanaotarajia kufanya mitihani yao ya kuhitimu kidato cha sita Mei 2024, wanatakiwa kuhakikisha elimu waliyoipata inakuwa chachu ya maendeleo katika jamii zao, na sio kwenda kuwa vikwazo kwa kujiingiza katika makundi yasiyofaaa.

“Walimu wenu wametumia muda mwingi kuhakikisha mnapata elimu hiyo lakini pia wazazi wametumia gharama kubwa ya kuwasomesha hivyo mnatakiwa kuwa mfano mzuri kwenye jamii na kuwa mfano bora wa kuigwa kwa wanafunzi wengine wanaoendelea na masomo,” amesema Nyamanza.

Aidha, Mwenyekiti Nyamanza pia aliendesha Harambee kwa kushirikiana na Wazazi, Viongozi wa dini, Walimu pamoja na Wageni waalikwa na kiasi kilichopatikana kilielekezwa  kukarabati Kanisa lililopo jirani na shule ya Sekondari Nyakato.

Mahafali hayo, yameshirikisha shule zote za Sekondari zenye wanafunzi Wasabato ambao walishiriki kwa pamoja kuwaaga wanafunzi wenzao wanaotarajia kuhitimu kidato cha Sita, ikiwemo shule ya Sekondari Nyakato, Ihungo, Kahororo, Rugambwa, Kagemu, Bukoba Sekondari, Mugeza, Buhembe, Maruku na Bakoba.

Simba SC yamshughulisha Kocha Mashujaa FC
Mkataba wa Kepa kusitishwa Real Madrid