Klabu ya Real Madrid haitarajiwi kumbakisha Kepa Arrizabalaga hadi mwisho wa mkopo wake wa sasa, na hiyo inamaanisha kwamba, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 atarejea katika klabu mama ya Chelsea msimu huu wa joto.

Kepa alijiunga na Madrid Agosti kama mbadala wa Thibaut Courtois ambaye aliumia, goti lake la kushoto.

Lakini kupewa nafasi na kocha Carlo Ancelotti, Kepa alijikuta akipoteza nafasi kwa Andriy Lunin tangu Novemba na hajapata nafasi tena.

Huku Courtois akitarajiwa kurejea uwanjani msimu ujao, baada ya kuona kurejea kwake kumecheleweshwa kutokana na jeraha, hivi karibuni Madrid haitamuhitaji Kepa tena.

Fabrizio Romano aliripoti kwamba mpango huo huko Bernabeu ni kumwacha Juni na kuongezwa kwa mkataba wa Lunin.

Mkataba wa sasa wa Lunin raia wa Ukraine unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu ujao na 2025 pia ndio wakati mkataba wa Kepa huko Chelsea unamalizika.

Alikuwa namba moja pale Stamford Bridge baada ya kushindana na Edouard Mendy, lakini The Blues wakamleta Robert Sanchez kutoka Brighton & Hove Albion kwa mkataba wa thamani ya pauni mnilioni 25 na kufungua njia kwa Kepa kuondoka na kutua Madrid, huku huko mwanzo aliripotiwa kutakiwa na Bayern Munich.

Hata kama Sanchez hatachukuliwa kuwa mchezaji wa muda mrefu, Chelsea bado wanahusishwa na Aaron Ramsdale, ambaye anatarajiwa kupatikana baada ya kupoteza nafasi yake Arsenal, na bado wanaweza kumfikiria Djordje Petrovic.

Nyamaza: Nendeni mkalete mabadiliko kwenye jamii
Twaha Kiduku: Nitamchakaza Harpreet Singh