Mshambualiji kutoka nchini Ureno na Klabu Bingwa nchini England Manchester City Bernardo Silva ana nafasi kubwa ya kuikacha klabu hiyo, itakapofika mwishoni mwa msimu huu 2023/24.

Silva mwenye umri wa miaka 29, kwa muda mrefu amekuwa kitaka changamoto ya kufikiria wapi atakapocheza msimu ujao, licha ya kuwa na mkataba na Man City hadi mwaka 2026.

Taarifa zinaeleza kuwa Mshambuliaji huyo ameshinikiza kuuzwa mwishoni mwa msimu huu, huku FC Barcelona ikitajwa kumuwania ili kuboresha kikosi chake, ambacho kinaelekea kupoteza ubingwa wa La Liga mikononi mwa Real Madrid.

Kocha Xavi anatajwa kuwa msukumo mkubwa wa kumvuta Silva kujiunga na FC Barcelona, japo inatajwa kama tetesi kuhusu wawili hao kuwa na mazungumzo.

Hata hivyo inatajwa kuwa FC Barcelona huenda ikawalazimu kutoa Pauni Milioni 50, kama ada ya uhamisho wa Bernardo Silva, ambaye alisajiliwa Man City mwaka May 06, 2017 kwa ada ya Euro Milioni 50 sawa na Pauni Milioni 43.5 kwa wakati huo.

TPBRC yateuwa Kamati ya Rufaa
Julian Alvarez: Ubingwa upo mikononi mwetu