Ule wimbo unaosikika mtaani wa ‘pesa kupotea mifukoni’ haumhusu Bosi wa WCB, Diamond Platinumz anayeendelea kuzihesabu ‘deals’ kubwa zaidi za matukio ambayo dunia nzima inayaangalia kwa macho yote.

Siku chache baada ya kutumbuiza kwa ustadi mkubwa kwenye tuzo za CAF jijini Abuja nchini Nigeria, Diamond amealikwa kutumbuiza kwenye ufunguzi wa Kombe la Mataifa ya Africa 2017 (AFCON 2017), Januari 14 nchini Gabon.

Chibu Dangote amewapa habari hiyo njema mashabiki wake kupitia mitandao ya twitter na Instagram, kwa kupost taarifa ya show yake hiyo iliyowekwa kwenye akaunti maalum ya AFCON 2017.

“GABON!!! You know we gat to make a World History on the 14th January right?? See you this this Coming Weekend then…? #WcbWasafi” aliandika.


Ingawa Tanzania haipo miongoni mwa nchi zinazoshiriki kombe hilo kubwa zaidi la soka barani Afrika, mwaka huu bendera itapeperushwa kupitia tasnia ya Muziki na kuiacha alama ya Tanzania kwenye mashindano hayo.

Millard Ayo aanza kazi ‘Citizen TV’ ya Kenya
Wakenya wamchezesha Nyota Ndogo Muziki wa Darassa, wamuitia pesa