Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ,Anthony Mtaka ametoa muda wa miezi mitatu kwa Wakala wa maji safi na mazingira Vijijini (RUWASA) kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa miradi ya  maji mkoani Dodoma.

Amesema hayo katika hafla ya kupokea mabomba kwa ajili ya utekelezaji wa mpango wa malipo kwa matokea awamu ya nne kimkoa.

RC Mtaka amewataka RUWASA kuhakikisha wanauwaunganishia maji wananchi wa maeneo  yote yaliyopo kwenye mpango huo ndani ya muda wa miezi mitatu vinginevyo watawajibishwa kisheria .

“Takukuru wapo hapa na  Jeshi la Polisi wapo hapa ,Sisi tumealikwa kwa nia njema kabisa  kuja kushuhudia kazi hii nzuri ,sasa baada ya miezi mitatu hawa ambao umewakaribisha kuja kushuhudia hafla hii watageuka sasa kuanza kuwashughulikia ninyi  kama mkishindwa ,sijui kama ninaeleweka ”amesema Mtaka .

Hata hivyo ameeleza kuwa lengo la kutoa vifaa hivyo ni kuondoa tatizo la maji maeneo hayo ambalo limekuwa la muda mrefu hivyo nia njema hiyo isiharibiwe na watendaji  wachache wazembe .

Awali akitoa taarifa  ya utekelezaji wa maradi huo Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Dodoma ,Dk.Godfrey  Mbabaye amesema kuwa mambomba hayo yana urefu wa mita 35,232  yenye vipenyo mbalimbali .

”Mpango huo utarejesha huduma ya maji  katika vituo 2,059  visivyotoa huduma hiyo katika wilaya hizo na utawanufaisha wananchi 1,324,255 sawa na asilimia 61.9 ya wakazi 2,139,450 waishio maeneo ya Vijijini katika Mkoa wa Dodoma”amesema Dk.Mbabaye.

Kwa upande wake  Mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini ,Anthony Mavunde amesema kuwa kuna baadhi ya miradi iliyokuwa ikitekelezwa na Wizara ya Maji kupitia mradi wa DDCA haikufanya vizuri kutokana na kushindwa kukamilishwa kwenyei jimbo  lake.

”Kuna miradi 13 ya maji ambayo inatekelezwa Jijijni hapo lakini kuna baadhi imekwama kutokana na kukwamishwa na rasilimali fedha ambazo zilikuwa zikitolewa na wahusika wa utekelezajiwa mradi”amesema Mavunde

Uturuki kushindwa kustahimili wahamiaji wa Afghanistani
Habari kubwa kwenye magazeti leo, Augusti 22, 2021