Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema kuwa imeamua kushirikisha taasisi zingine za kimataifa ili kuwachunguza baadhi ya watuhumiwa wa Escrow kama wamehifadhi fedha nje ya nchi.

Hayo yamesemwa na Afisa Habari na Uhusiano wa taasisi hiyo, Mussa Misalaba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, ambapo amesema kuwa watuhumiwa wote wa Escrow bado wanaendelea kuchunguzwa.

Amesema kuwa Takukuru inaendelea kuwachunguza watuhmiwa wote huku ikishirikiana na baadhi ya taasisi za nje na kwamba uchunguzi huo unafanyika kwa umakini zaidi ili haki itendeke.

“Hili jambo linafanyika kwa umakini mkubwa, usione kimya kuna jambo linafanyika, kwa sasa ni mapema sana kusema chochote kuhusu jambo hili kwakuwa linahitautlivu mkubwa kulishughulikia,”amesema Misalaba

Aidha, hivi karibuni TAKUKURU iliwafikisha mahakamani baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi na uhujumu uchumi ili kujibu mashtaka yanayowakabili.

Hata hivyo, waliofikishwa mahakamani kujibu tuhuma ni pamoja na Theofilo Bwakea, Mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engineering and Markerting, na aliyekuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya IPTL, James Rugemalila wote wakikabiliwa kesi ya uhujumu uchumi

 

Lukaku afunguka alivyoiota Manchester Utd
Mzee wa Upako ampiga tafu Q chillah