Dhoruba ya kitropiki ya Gamma, ambayo imeathiri sehemu za kusini mashariki mwa Mexico, imeua watu 6 na kuhamisha maelfu ya watu.

Maafisa wamesema kuwa dhoruba ya kitropiki imeathiri mwambao wa Peninsula ya Yucatan na majimbo ya Tabasco na Chiapas kwa upepo mkali na mvua.

Katika taarifa iliyotolewa na wakala wa ulinzi wa raia wa Mexico, imeripotiwa kuwa watu 4, ambao walikuwa watoto 2, wamefariki katika maporomoko ya ardhi yaliyosababishwa na dhoruba ya kitropiki ya Gamma huko Chiapas.

Taarifa hiyo imesema kwamba dhoruba hiyo ya kitropiki imeathiri zaidi ya watu nusu milioni katika sehemu za Yucatan na jimbo la Chiapas, na imeelezwa kuwa zaidi ya watu 3,400 makazi yao yameharibiwa.

Lady Jay Dee matatani, adaiwa kuhamasisha matumizi ya bangi
Chanzo cha ajali iliyoua watano Dar