Jeshi la Chad limesema limewapokea jumla ya Wanajeshi 320 wa Sudan waliotoroka mapigano makali nchini mwao kati ya wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka – FSR, na jeshi la serikali waliovuka mpaka na kujisalimisha.

Jenerali Daoud Yaya Brahim akiambatana na mawaziri kadhaa, amesema “wanajeshi hawa waliingia katika ardhi yetu, wote walinyang’anywa silaha na kugawanywa sehemu nne na kuna maafisa wa polisi na wanajeshi 320 wa vikosi vya usalama na jeshi kutoka Sudan ambao wanahofia kuuawa na kikosi cha RSF ambao walijisalimisha kwa vikosi vyetu.”

Hata hivyo, Brahim kutoa maelezo zaidi ikiwa ni pamoja na wapi hasa walivuka mpaka katika siku ya tano ya mapigano kati ya vikosi vya majenerali hao wawili ambao hadi wakati vita ilipozuka walikuwa akigawana madaraka huko Khartoum na mapigano haya yameua zaidi ya raia 270 hadi sasa, maelfu ya wakazi wakitoroka kufuatia mashambulio ya mabomu katika mji mkuu wa Sudan.

Mapigano hayo bado yanaendelea kati ya FSR ya Jenerali Mohamed Hamdane Daglo, anayejulikana kama “Hemedti”, na jeshi linaloongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhane, katika anayeshikilia mamlaka tangu mapinduzi yao ya kijeshi ya mwaka 2021.

Chad, ilifunga mpaka wake na Sudan siku ya Jumamosi, eneo lenye urefu wa zaidi ya kilomita elfu moja katikati ya jangwa, na inapakana na Darfur, magharibi mwa Sudan. Mpaka huu wenye vinyweleo vingi huvukwa mara kwa mara na waasi kutoka nchi zote mbili.

Habari Kuu kwenye magazeti ya leo Aprili 21, 2023
Sadaka ya mfungo yaleta maafa, 78 wafariki kwa kukanyagana