Makumi elfu ya watu wanatarajiwa kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Hayati Papa Benedict XVI huko Vatcan.

Mapema leo asubuhi watu walianza kukusanyika kwenye viunga vya St. Peter’s Square tayari kutoa heshima za mwisho kwa kiongozi huyo aliyefariki Desemba 31, 2022 akiwa na umria wa miaka 95.

Mazishi ya kiongozi huyo mstaafu wa Kanisa Katoliki Dunia yanatarajiwa kufanyika Alhamisi ambapo yataongoza na Papa Francis, ikiwa ni mara ya kwanza kwa Papa kuzikwa na mrithi wake.

Mwili wake utawekwa katika jeneza la wazi kwa siku tatu katika Kanisa la Basilika la Mt. Petro mjini Roma ambalo ni kanisa kubwa kuliko yote duniani na hutumiwa sana na Papa.

Habari Kuu kwenye magazeti ya leo Januari 3, 2023
AU yaitaka Rwanda kutowaunga mkono M23