Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF), umesema umeridhishwa na utekelezaji wa Mradi wa
Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia (EBARR) unaotekelezwa katika
Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma, na kusimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais.

Hayo yamesemwa hii leo Jumatano (Februari 15, 2022) na ujumbe wa Mfuko huo ukiongozwa na
Mratibu wa GEF Kanda ya Afrika, Dkt. Ibrahima Sow wakati wa ziara ya kutembelea Mradi huo
katika Vijiji vinne vya Wilaya hiyo.

Ujumbe wa GEF ukiongozwa na Mratibu wa Kanda ya Afrika, Dkt. Ibrahima Sow (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja wakati walipotembelea mradi wa maji wa safi na salama unaoratibu na Mradi wa EBARR ulio chini ya usimamizi wa Ofisi ya Makamu wa Rais katika Kijiji cha Kiegea Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma leo Jumatano (Februari 15, 2023).

Amesema, GEF imedhirisha na utekelezaji wa miradi hiyo ambayo ni ujenzi wa visima
virefu vinne, malambo mawili, majosho mawili, vitalu nyumba vitatu na mashine ya kukamulia
alizeti ambapo miradi hiyo imeweza kuwa chanzo mbadala cha kuongeza kipato kwa wananchi.

“Miradi hii ina faida kubwa kwa wananchi wa Mpwapwa, natoa rai kwa jamii kuweza kuitunza
na kuwasaidia kwa ajili ya kuleta manufaa ya sasa na kwa kizazi kijacho” amesema Dkt. Sow
ambaye aliambatana na ujumbe kutoka Sekretarieti ya GEF.

Afisa Mazingira Mwandamizi wa Mabadiliko ya Tabianchi kutoka Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF) Filippo Berarch akitazama mbegu za alizeti zinazotumika kwa ajili ya kutengeneza mafuta na mashudu ya vyakula vya mifugo wakati wa ziara ya ujumbe huo kukagua Mradi wa EBARR unaotekelezwa na kusimamiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais wakati wa ziara ya ujumbe huo leo Jumatano (Februari 15, 2023) Wilayani
Mpwapwa Mkoani Dodoma.

Sow ameongeza kuwa, GEF itaendelea kufadhili miradi ya mazingira inayozunguka jamii ili kuongeza
kasi ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira katika maeneo ya vijijini sambamba kuhakikisha
jamii inajishughulisha na kilimo rafiki kwa mazingira na kutolea mfano kilimo cha mbogamboga.

Kwa upande wake, Mratibu wa Mradi wa EBBAR Kitaifa, Dkt. Makuru Nyalobi amewataka
wananchi wa Wilaya hiyo kusimamia vyema miradi hiyo ya maendeleo inayotekelezwa katika
maeneo yao ambayo inatarajia kuwanufaika wananchi wa vijiji vya Nghambi, Mbugani, Kiegea
na Kazania.

Dkt. Tax na ujumbe wa Tanzania mkutano wa Mawaziri AU
Wateule wa Rais Samia wala kiapo Ikulu