Taifa la Urusi limeapa kutimiza malengo ya uvamizi wake wa kijeshi nchini Ukraine bila kujali chochote kitakachotokea

Rais wa Urusi Vladimir Putin ambaye aliwahi kuwa mwanajeshi amemwambia Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kuwa nchi yake itayafikia malengo yake kwa Ukraine bila kutishwa wala kuyumbishwa.

Kupitia kwa taarifa baada ya marais hao wawili kuzungumza kwa njia ya simu, Kremlin iliweka wazi malengo ya uvamizi wake yanayojumuisha kumaliza silaha hatari za Ukraine na taifa hilo pia kutoegemea upande wowote.

“Vladimir Putin ametoa maelezo ya kina kuhusu mfumo na masharti ya mazungumzo na maafisa wa utawala wa Kyiv. Pia imethibitishwa kwamba, kwanza kabisa, tunazungumzia kumalizwa kwa silaha hatari za Ukraine na taifa hili pia kutoegemea upande wowote ili iwe kwamba hatari yoyote kwa Urusi haitawahi tokea katika eneo lake,” ilisema taarifa ya Moscow.

Taarifa hiyo imesema kuwa juhudi zozote za kuchelewesha mazungumzo kati ya maafisa wa Urusi na Ukraine kutawafanya utawala wa Moscow kuongeza masharti zaidi.

“Ilisisitizwa pia kuwa malengo ya oparesheni ya kijeshi yatatimizwa na juhudi zozote za kupata muda zaidi kwa kuchelewesha mazungumzo kutasababisha Urusi kuongeza masharti kwa utawala wa Kyiv katika mazungumzo yetu,” taarifa hiyo iliongeza.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo oparesheni ya Urusi nchini Ukraine ilikuwa inaendelea jinsi ilivyopangwa na kutarajiwa.

Urusi inataja uvamizi wake kama oparesheni maalumu ikisema kuwa hailengi kumiliki Ukraine bali kumaliza uwezo wa kijeshi wa Ukraine na kunasa kile inachodhani ni hatari kwa usalama wake.

Rais ateta na Baraza la Mawaziri
Aliyesema alipewa kitita cha bilioni 2.1 na Mpenziwe agundulika ni mhalifu wa kimataifa wa kifedha