Rais wa Zambia, Hakainde Hichilema amempongeza Rais Mteule wa Kenya William Ruto kwa ushindi wake katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9, ambao umeidhinishwa na Mahakama ya Juu.

Dakika chache baada ya Mahakama ya Juu kutoa uamuzi wake, Rais Hichilema aliingia kwenye mitandao ya kijamii kumpongeza kwa ushindi huo na kumhakikishia Ruto kuwa uhusiano wa nchi hizo mbili utaimarishwa.

Jaji wa Mahakama ya juu nchini Kenya, Martha Koome.

“Hongera Dkt. William Samoei Ruto, kwa kutangazwa kuwa Rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya,” ameandika Rais Hichilema.  

Amesema, “Tunatarajia kufanya kazi na Mheshimiwa William Ruto, ili kuimarisha na kuimarisha uhusiano mzuri wa kihistoria kati ya Zamibia na Kenya, kulingana na vipaumbele vyetu vya pamoja kwa watu wetu wawili.”

Majaliwa ataka kasi na viwango kwa Wakandarasi wa barabara
Kenya: Mahakama yakubali ushindi wa Ruto