Jukwaa huru la wazalendo limelaani kitendo cha  meya  wa jiji la  Dar  es salaam  ndg Mwita Waitara cha kuwapotosha kwa makusudi wanainchi wa Dar es salaam na taifa kwa ujumla kuhusu agizo la   mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Makonda la kuchukua taarifa za kila kaya.

Hayo yamesemwa na Mw/kiti wa jukwaa hilo Bw,Andrew Kadege alipokuwea akiongea   na waaandishi wa  habari  jijini Dar es salaam mapema hii leo,na kuongeza kuwa jukwaa limesikitishwa sana na kuibuka kwa ndugu Mwita na harakati za kupinga hatua hiyo nzuri ya Mh, Makonda kutaka kujua taarifa za kila kaya.

Aidha alionngeza kuwa  harakati za kisiasa za ndg Mwita zimemshtusha ata  mlezi wa chama hicho  ndg Edward Lowasa na kukemea siasa za kiharaakati ambazo zinapinga maendeleo ya nchi,’’jukwaa linakemea vitendo aambavyo vinarudisha nyuma jitihada za serikali ya awamu ya tano  na kuchelewesha uhakiki wa wanai nchi  wake’’ alisema Bw, Kadege.

Hata hivyo jukwaa imemtaka meya kutokuendelea na tabia ya kuwalaghai wanainchi kutoshiriki katika shughuli za maendeleo kwani ndio sehemu yao ya kujikwamua kiuchumi  na kuondoa umasikini unaowakabili watanzania kwa ujumla.

Jukwaa limeongeza  kuwa hatua hiyo ya mkuu  wa mkoa  wa Dar es salaam ya kutaka kuwatambua  wainchi wa  mkoa wake wa Dar es salaam katika ngazi  ya kaya ni kutaka  kujua  jinsi gani ya kuweza kupanga na kuwahudumia kama ilivyo katika majiji  ya London,Paris na Berlin inavyofanyika.

Jukwaa huru limechukua nafasi hiyo kuwaomba na kuwashauri wanainchi wote popote litakapo fanyika  zoevzi hilo  kushirikiana na serikali kikamilifu kwani ni kwa manufaa ya wainchi wenyewe na taifa kwa ujumla ili kuweza kuinua uchumi.

Serikali Imekitoza Faini Kiwanda cha Sabuni (Royal Soap industry).
Waziri Mkuu Apiga Wanafunzi Kutumia Viberiti, Mishumaa Mabwenini